"Miasha ni zawadi . Ifurahie. Maisha ni safari, uwe na mwelekeo(malengo)"
Maisha yana maana unapojitambua wewe ni nani na ukaishi
kadiri ya uhalisia wako. Kujitambua ni kupana mno. Mtu anaanza kujitambua akiwa
tumboni mwa mama na anapozaliwa anaendelea kujitambua.
Kujitambua hakuna ukomo, hakuna kuhitimu ndiyo kusema maisha
ni kujifunza kila siku ya Mungu. Binadamu anajifunza mpaka siku anayorejea kwa
muumba wake. Ukomo wa kujitambua ni kifo. Anayekoma kutaka kujitambua angali
hai huyo ni mfu anayeishi.
Blog hii ni sehemu ya wewe kufahamu kwa nini unaishi.
Unaishi kwa sababu zipi na dunia inanufaika vipi na uwepo wako hapa
ulimwenguni. Hii ni blog ya kukufanya uishi kwa malengo, na kuacha kuishi kwa
mazoea. Ukiwa msomaji wa blog hii kila siku utaiona siku ya thamani na
hautaitumia kwa hasara na hatimaye maisha yako yatakuwa ya mafanikio.
Tiba mbadala ya tabia hasi. Kuna watu wengi wamekwama katika
tabia zenye matokeo mabaya kwenye maisha yao. Wamejizoesha tabia zenye kuathiri
ustawi wao wa kiroho, kiakili na hata kimwili. Blog hii ni sehemu sahihi kwako
uliye katika changamoto za kimwenendo. Hii ni hospitali yako.
Yako maradhi ambayo hayatibiki hospitalini lakini
yanadhurumu maisha ya watu na familia nyingi. Kadiri utakavyotembelea blog hii
utatibika pia utajigundua kama wewe ni muhanga.
Furaha ni haki na zawadi yako. Maisha yafaa nini kama huna
furaha moyoni mwako. Furaha huumbwa, huambukizwa. Blog hii kama ilivyo jina
lake ni chemchemi ya furaha. Msomaji wa blog hii hapa ndipo penye chemchemi
nzuri ya raha na amani.
Wakati watu wengi
wanatumia starehe hatarishi ili wapate furaha matokeo yake bado wanajikuta
wanapungukiwa. Mimi nakushauri kuwa msomaji wa blog hii na utakuwa na furaha
tele. Tena furaha halisi ya kutoka ndani.
Kuna watu wanatazama maisha kwa macho ya kijuu juu blog hii
itakufanya ufahamu zaidi ya unavyofahamu. Maisha yako hayatakuwa kama jana
baada ya kuwa msomaji wa blog hii. Kama muendeshaji wa blog niseme tu nakupenda sana.
KARIBU CHEMCHEMI3.BLOGSPOT.COM NI DARASA LA MAISHA. KLINIKI
YA MAISHA YAKO
Post a Comment