“Kwa kitaalamu, ugonjwa wa akili ya ngono wa kupenda
kuacha mwili wazi unaitwa ‘exhibitionism’ ambapo mtu huweza kuamua kuacha
maziwa, mapaja au kwa wanaume kuvaa suruali inayoelekea kuanguka kutoka
maungoni,” Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akili na mtaalamu wa waathirika wa
dawa za kulevya, Augustine Godman
Kwa ufupi
·
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akili
na mtaalamu wa waathirika wa dawa za kulevya, Augustine Godman anasema, magonjwa
ya akili kwa ujumla wake yanaweza kuzidi 1,886 lakini yapo yale ya ngono ambayo
pengine yana changamoto lukuki kwa mwanadamu hasa Watanzania wasiofahamu kuwa
ni magonjwa ya akili.
Huenda tumewaona
wengi wao kama mashujaa, vijana wa kisasa au hata dada zetu wanaokwenda na
wakati, kumbe ni wagonjwa wa akili.
Unasikiliza
taarifa ya habari jioni. Unasikia kuwa, mwanamume amembaka mtoto wa miezi
mitatu. Unaihoji nafsi yako… ni jambo gani lililosababisha akafanya ukatili huo?
Je, ni tamaa kali ya ngono?
Wengine hudhani ni
kisasi au imani za kishirikina na kwamba wahusika wametumwa.
Huu ni upotoshaji,
lakini ukweli ni kuwa hayo ni magonjwa ya akili ya ngono ambayo yanawakumba
asilimia 35 au zaidi ya Watanzania wote.
Watanzania hawa
wanaugua magonjwa haya kwa wakati mmoja na kusababisha madhara mbalimbali
kijamii, kiuchumi na migogoro katika familia na katika uhusiano.
Watu wenye
magonjwa haya, si lazima watembee wakiokota makopo, kuvua nguo au kuwa na
nywele ambazo hazijachanwa.
Hawa ni watu wa
kawaida ambao tunafanya nao kazi, wenye uwezo mkubwa katika taaluma au pengine
ni wazazi au hata walezi.
Daktari Bingwa wa
Magonjwa ya Akili na mtaalamu wa waathirika wa dawa za kulevya, Augustine
Godman anasema, magonjwa ya akili kwa ujumla wake yanaweza kuzidi 1,886 lakini
yapo yale ya ngono ambayo pengine yana changamoto lukuki kwa mwanadamu hasa
Watanzania wasiofahamu kuwa ni magonjwa ya akili.
Dk Godman
anafafanua kuwa magonjwa ya akili ya ngono kuwa ni yale yanayohusisha
athari , upungufu au mparaganyiko au vitu visivyo vya kawaida
katika tendo la ngono.
“Mtu anaweza kuwa
na matatizo ya kihisia au ya kisaikolojia au vya kitabia katika
suala la ngono na huweza kusababisha madhara au kutopata mafanikio,” anasema Dk
Godman
Daktari huyu
ambaye amewahi pia kufundisha Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba Muhimbili (Muhas),
kitengo cha magonjwa ya akili anasema watu wengi wana magonjwa ya akili
ya ngono, lakini hawajui kama ni magonjwa na wanaendelea kuishi hivyo
hivyo wakidhani ndivyo walivyo na baadhi wakipata matatizo katika jamii,
wengine kufungwa jela au kupigwa kutokana na tabia hizo.
Mara nyingi
tumekuwa tukiona wanawake wanavaa mavazi ya nusu uchi, wakizianika nje
sehemu kubwa za miili yao.
Tabia hizo
ambazo pengine huweza kuigwa na wengine ni miongoni mwa magonjwa ya
akili ya ngono kwani watu wanaopenda kufanya hivyo hujisikia raha na amani watu
baki au wageni wenye jinsi tofauti wanapoyaangalia maungo yao na kushtuka.
“Kwa kitaalamu,
ugonjwa wa akili ya ngono wa kupenda kuacha mwili wazi unaitwa
‘exhibitionism’ ambapo mtu huweza kuamua kuacha maziwa, mapaja au kwa wanaume
kuvaa suruali inayoelekea kuanguka kutoka maungoni,” anasema
Anasema, watu aina
hii hutosheka kimapenzi mara tu wanapoona wanaume au wanawake wengine wameyaona
maungo yao. Hata hivyo, anasisitiza kuwa hutosheka pale tu watu wageni
wanapoyaona maungo yao.
Mhadhiri wa
Sosiolojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Thomas Ndaluka anasema, baadhi ya
magonjwa haya yanasababishwa na historia ya mtu.
Anasema hata hivyo
mparaganyiko kama ule wa kupenda kuacha maungo wazi, unaambukiza kwa maana ya
kuwa, anayeanza kufanya hivyo ni mgonjwa wa akili na matokeo yake wengine
wanaiga.
Ubakaji wa watoto
wachanga
Wengi wamekuwa
wakihusisha ugonjwa huu na imani za kishirikiana, lakini ukweli ni kuwa, wale
wanaowabaka watoto wadogo au kuwalawiti wana matatizo ya akili ambayo kitaalamu
yanaitwa pedophilia (paedophilia).
“Katika hali ya
kawaida si rahisi mtu mzima akamtamani kimapenzi mtoto wa miezi mitatu,”
anasema mtaalamu huyo.
Ugonjwa huu
unatokea pale mtu anapokuwa na hali ya kupata raha ya ngono kwa watoto wadogo
wenye umri wa chini ya miaka mitano.
“Watoto wa jinsi
zote huweza kuathiriwa na tatizo hili. Mtu mwenye ugonjwa huu huweza kuamua
kumuingilia mtoto au tu kuamua kumchezea via vyake vya uzazi,” anasema Dk
Godman.
Mhadhiri wa
Saikolojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk Kitila Mkumbo anasema sababu kuu za
maradhi hayo ya akili ni pamoja na mazingira ya mtu wakati wa balehe, aliambiwa
nini kuhusu tendo la ndoa na makuzi yake kwa jumla.
“Kwa mfano
inategemea kijana anaambiwa nini wakati wa balehe au yeye mwenyewe anaelewa
nini maana ya tendo hilo” anaeleza Dk Mkumbo.
Anatoa mfano kuwa,
wapo baadhi ya wanaume wanaamini au kufananisha kila shimo na uke.
“Huu ni ugonjwa
mkubwa sana. Ndiyo maana utasikia mtu kambaka mbuzi. Yeye anaamini kila shimo
linaweza kutumika kama uke”, anasema
Anafafanua kuwa
magonjwa mengi ya akili ya ngono hujitokeza wakati wa balehe na hukua
kadri mtu anavyokosa matibabu.
Yapo matukio
kadhaa yaliyowahi kutokea hapa nchini yanayoeleza watu waliowabaka watoto
wadogo.
Kwa mfano, Desemba
2012, Yakobo Raymond alifikishwa mahakamani huko wilayani Muheza, Mkoani Tanga
kwa tuhuma za kumbaka mtoto wake wa kambo mwenye umri wa miaka mitatu.
Pia, huko mkoani
Arusha, mwezi Januari mwaka jana, David Samweli mkazi wa Moivaro Wilaya
ya Arumeru, aliwabaka watoto wawili wa kike wa jirani yake na mtoto wake
wa kumzaa kwa nyakati tofauti chumbani kwake.
Licha ya
matukio kama haya kuripotiwa zaidi kwa wanaume wenye tabia hii, Dk Godman
anasema wapo wanawake ambao pia huwabaka watoto wadogo wa kiume.
“Mwanamke anaweza
kumvua nguo mtoto mdogo na kuanza kumshikashika tu, hapo huwa amepata
raha yake. Lakini pia anaweza kuamua kumwacha mtoto akiwa uchi,” anasema
Mtu mwenye ugonjwa
huu humrubuni mtoto kwa vitu vidogo vidogo ili ampende na kumweka karibu naye
na wakati mwingine baada ya kumfanyia vitendo hivyo humtishia kuwa akisema,
atamdhuru.
Tafiti
mbalimbali zinaeleza kuwa, wapo watu katika nchi zilizoendelea ambao huasili
watoto, kisha kuwatendea vitendo hivi vya upedofilia.
Kufanya mapenzi na
maiti
Ni jambo ambalo
huzungumzwa au kutajwatajwa, lakini kumbe lina ukweli ndani yake.
Wengine wamekuwa
na hisia kuwa linahusiana na imani za kishirikina au utumiaji wa dawa za
kulevya lakini kumbe ni miongoni mwa magonjwa ya akili.
Wapo watu ambao
hujisikia raha ya ngono kwa kufanya mapenzi na maiti. Watu hawa kwa kitaalamu
huitwa ‘necrophilia’.
“Kwa kawaida ugonjwa
huu huwa hauripotiwi mara kwa mara kwa sababu ya hofu ya kukiri kuwa umefanya
mapenzi na maiti pia wanaotenda matendo hayo” anasema Dk Godman.
Dk Mkumbo anasema
kuwa magonjwa haya ya akili yana tiba ambazo zaweza kuwa ni za
kisaikolojia, sosholojia na kwa dawa.
“Kisaikolojia tiba
ya watu hawa ni kupewa unasihi wajue kuwa wao ni binadamu na waache tabia
ambazo kwa kawaida hazifanywi na binadamu” anasema Dk Mkumbo.
Kuwabaka wanyama
Hili limeshawahi
kuandikwa na vyombo kadhaa vya habari na kuwashangaza watu wengi duniani
ikiwemo pia katika Tanzania.
Zipo ripoti kadhaa
za watu kuwabaka wanyama hasa wale wafugwao kama kuku, mbuzi, farasi na ngombe.
Kwa mfano,
Kijana mmoja mkazi wa mkoa wa Tanga alifikishwa mahakamani kwa tuhuma ya
kumbaka na kumwingilia kinyume cha maumbile mbuzi wa jirani yake.
Katika tukio
jingine, Yusuph Bakari mkazi wa Kata ya Kigera, Manispaa ya Musoma Mkoani Mara
alinajisi kuku jike na kumsababishia maumivu makali na kusababisha afikishwe
kwa afisa mifugo kwa uchunguzi zaidi.
Aliyekuwa Kamanda
wa Polisi wa Mkoa huo, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Absalom Mwakyoma
alithibitisha tukio hilo.
Huu ni
miongoni mwa magonjwa ya akili ya ngono na kwa kitaalamu ugonjwa huu unaitwa
zoophilia na ni kosa la jinai katika nchi nyingi ikiwemo Tanzania.
Ndani ya daladala
Wanawake
wengi wamekuwa wakilalamika kuwa wanapopanda katika magari ya abiria hasa
nyakati za asubuhi au jioni pindi mabasi yanapokuwa yamejaa kupindukia, wapo
wanaume ambao huwasogelea na kuwabana kwa kiasi kikubwa.
“Basi kama
umewahi kukutana na hali hiyo ujue umekutana na wanaume wenye ugonjwa wa akili
uitwao ‘ufroteri’. Ugonjwa huu wa akili huwakumba zaidi wanaume ambao hupenda
kujisugua via vyao vya uzazi kwa watu wasio na ridhaa.
“Mara nyingi
hutokea katika maeneo ya umma, au yenye msongamano. kila wanapogundua kuwa
wameonekana wakifanya tendo hilo, hisia zao huisha hapo hapo na huondoka,”
anasema mtaalam huyo.
Anasema,
mara nyingi watu hawa si kuwa hawana wenza bali wanapata hisia zaidi
wanapojisugua katika maumbile ya mwanamke ambaye hafahamu nini kinaendelea.
Kipigo, majeraha
Umeshawahi
kupata tetesi za wanawake ambao kila mara huamka na majeraha makubwa usoni na
mwilini?
Usishangae kusikia
kuwa mwanamke huyo ana mwenza mwenye matatizo ya akili ya ngono.
Upo ugonjwa wa akili
ya ngono ambao unahusisha vitendo halisi vya kujeruhi au kusababisha maumivu au
kutoa manyanyaso.
“Kinachompa raha
ya tendo hilo ni kumpiga mwenza wake, kumtukana wakati wa tendo au kumjeruhi,
kumng’ata na kumuona akilia kwa uchungu au akitoka damu,” anasema Dk Godman.
Mtaalamu huyo
anasema hali hii inapozidi huweza kusababisha mauaji au majeraha ya
kudumu na watu wengi hudhani ni manyanyaso ya kijinsia ya kawaida.
Dk Ndaluka
anasema watu wengi wa kundi hili wamepata maradhi hayo kutokana na historia za
maisha yao.
“Wengine waliwahi
kubakwa, kuteswa au kufanyiwa vitendo kama hivi na hawakupata msaada wa
kisaikolojia kuondoa ule uchungu. Hivyo wanaweza kuwa na matatizo haya
kiufahamu” anasema
Hapa Dk
Ndaluka anasema hatua za kisheria zinahitaji kuchukuliwa ili kumlinda mwenza
ambaye huathiriwa.
Kupiga chabo
Upo ushahidi kuwa
baadhi ya vijana hudiriki kutoa fedha kwa walinzi au wahudumu wa nyumba za
wageni ili wawape ruhusa ya kuangalia watu wanaofanya mapenzi
katika vyumba.
Lakini tofauti na
wengi wanavyofikiri huu si ukosefu wa maadili tu, bali ni ugonjwa wa akili ya
ngono ambao mtu hupenda kuwaangalia watu wanaofanya mapenzi, ambao ni wageni
machoni pake (si ndugu wala jamaa) na kukamilisha raha ya ngono. Kwa
kitaalamu ugonjwa huu wa akili huitwa ‘voyerism’.
Kwa mfano,
Mhudumu wa Nyumba ya wageni ya Savannah iliyopo Tabata, Ndosi
Yakobo anakiri na kusema kuwa vijana huomba kuja kuwachungulia wapenzi
wanaoingia humo.
“Ieleweke kuwa
watu wa aina hii hawana nia ya kufanya ngono na watu wanaowachungulia, na
wanapogundulika tu kuwa wanafanya hivyo zile hisia huisha papo hapo,” anasema
Watalaamu wa
magonjwa ya akili wanaeleza kuwa watu wa kundi hili wanaweza pia kupenda
kuwatazama watu wakivua nguo au watu waliokaa utupu.
Mapenzi kwa njia
ya simu
Wapo watu ambao
hupata hisia za ngono kwa kuzungumza lugha ya matusi inayohusisha viungo vya
mwili au vitendo vya kingono.
Huu ni ugonjwa wa
akili ambao baadhi ya watu wanao pasipo kujua kuwa ni ugonjwa.
Baada ya
teknolojia ya simu kuvumbuliwa, ugonjwa huu umekithiri na sasa watu wenye
tatizo hilo wanatumia simu kufanya mapenzi au kuzungumza lugha ya matusi, kisha
kupata hamu ya mapenzi.
Kitaalamu, mapenzi
kwa njia ya simu huitwa, ‘telephone scatologia’ na hivi sasa watu wanaweza
kujiunga na huduma fulani ambayo huzungumza njia za kufanya ngono au jinsi ya
kumfurahisha mwenza na kumbe kwa njia hiyo watu wanatimiza haja zao.
Ugonjwa mwingine
unaoendana na huu ni ule wa kupata hisia za ngono kwa njia ya mitandao ya
kijamii. Wanatumia intaneti kuzungumza habari za ngono hadi wanatimiza
haja zao.
“Huu ni ugonjwa
unaoathiri zaidi na unawaathiri vijana. Mara nyingi wakianza hawawezi kuacha
hadi watibiwe,” anasema Dk Godman.
Hata hivyo, Dk
Godman anaeleza kuwa yapo magonjwa mengine ya akili ya ngono madogo madogo
ambayo yanaathiri watu wengi kwa mfano wapo watu wana mwamko mkubwa mno wa
tendo la ngono kiasi cha kushindwa kulala wasipofanya hivyo.
Dk Ndaluka
anasema ni wakati sasa watu kupata ushauri wa kisaikolojia na matibabu na
wakubali kuwa haya ni magonjwa ya akili na siyo tabia.
Naye Dk Godman
anasema kutokana na uelewa mdogo wa magonjwa ya akili ya ngono watu wengi
wamefungwa kwa sababu ya kuwajeruhi wenza wao nakuwabaka watoto wadogo.
Dk Mkumbo anashauri
kuhusu ugonjwa wa akili wa kuwabaka watoto (paedophilia) na kusema kuwa watu
kama hawa wanaweza kuwa hatari katika jamii hivyo wanahitaji matibabu.
Anashauri
kuwa wazazi wawalinde watoto na waache tabia ya kuacha mtoto apakatwe au
kuogeshwa na kila mtu.
“Hawa mapedophilia
ni wengi hapa nchini, bila kupewa matibabu na sheria kuchukuliwa watoto wengi
wapo hatarini” anasema
Anasema
licha ya matibabu ya kisaikolojia pia wagonjwa hawa huweza kupewa dawa za
kupunguza kiwango cha vichocheo
elimu hii ni ya muhimu sana ienezwe zaidi.
ReplyDeletetatitizo la kuangalia picha za ngono kwenye mitandao au simu za mikononi ni la ugonjwa gani?
ReplyDelete