Banner Huu ndiyo wakati wa ndoto zako | Darasa La Maisha - Maisha Mafanikio

0


               Kila dakika ina thamani sababu ikitumika  hauwezi kuirudisha” Willie Jolley

Upo hivyo ulivyo na hapo ulipo kadiri ya matumizi yako yaa muda. Na kesho utakuwa kadiri ya matumizi yako ya muda huu ulionao leo. Muda hauamui hatima ya maisha ya mtu, muda hautimizi ndoto za mtu bali matumizi yako ya  muda ndiyo yanaamua hatima ya maisha yako.

Vile unavyotumia muda vizuri kwa kufikiria mambo ya msingi na kupanga mipango ya kimaisha unayotaka kuitimiza ndivyo utakavyofanikiwa. Kadiri  unavyotumia muda wako katika kujibidiisha kumuomba Mungu ndivyo utakavyofanikiwa. Kadiri unavyoepuka kufanya mambo yasiyo na tija kwa afya yako, na katika maendeleo yako ndiyo utakavyofanikiwa.

Kama wewe ni mtu ambaye unatumia muda mwingi kulaumu wazazi, ndugu, marafiki, na serikali kwamba ndiyo sababu ya wewe kutofanikiwa katika hali mbalimbali za kimaisha, unakosea sana na unaendelea unapoteza muda. Kabla ya kulaumu watu wengine jichunguze kwanza matumizi yako ya muda kisha ujilaumu wewe mwenyewe.

Jilaumu kwa kutokuwaza vizuri kwa wakati, jilaumu kwa kwa kutofanya maamuzi mazuri kwa wakati sahihi, jilaumu kwa kutokutenda kwa wakati. Ulishindwa kucheza na muda vizuri. Kabla ya kumlaumu mtu mwingine unayehisi amehusika katika kukukwamisha kufikia kilele cha ndoto zako jikague matumizi yako ya muda.

 Jilaumu kwa kwa kutumia muda mwingi kupiga soga, kuongea na simu, jilaumu kwa kupoteza muda kwenye mahusiano ya kimapenzi ambayo yamekushushia heshima, jifinye kwa kupoteza muda mwingi kitandani badala ya kupambana na changamoto za maisha, jilaumu kwa kwa kupoteza muda kwenye mitandao ya kijamii(facebook, twiter, bmm, whatsup na instagram) badala ya kufanya mambo yatakayokunufaisha. Pia usipoteze muda kwa kujilaumu tu kwa makosa yaliyopita,fikiria jambo jipya.

Hakuna muda usio na jambo la kufanya. Hivyo mtu akisema wiki nzima, siku saba za wiki hana cha kufanya anajidanganya mwenyewe. Ni dalili tu ya uvuvu, kujionea huruma, kujibweteka na kutojitambua na wakati mwingine kufikiri umeshafanikiwa vya kutosha.

Mvivu analala hata saa kumi na sita kwa siku hivyo kujikuta ana saa nane tu za kazi. Wakati kiafya inashauriwa saa nane zitumike kulala kumi na sita zitumike kwenye kazi. Usikae bure, usiache kupumzika lakini usiache kutumia muda vizuri, ni nyenzo nzuri ya mafanikio.

Ili ufanikiwe katika maisha, lazima ufahamu wewe ni nani na nini unataka maishani mwako. Hivyo kuna muda wa kujitambua, kuna muda wa kutafakari nini unataka, kuna muda wa kukiombea unachokitaka, kuna muda wa maandalizi wa kile unachokitaka kadhalika kuna muda wa kukiita unachokitaka kwa vitendo.

Mungu ni mwenye haki, ametoa saa 24 za siku kwa kila mtu, maskini ana saa 24, tajiri ana saa 24. Msomi na asiye na elimu wote wana saa 24. Kinachotutofautisha ni vile tunatumia hizo saa 24 za siku.   Wanaozitumia vizuri wanatoka, wanaozitumia vibaya wanakwama. Hata leo umepewa saa 24 mikononi mwako, unazitumiaje ndivyo utakavyokuwa kesho.
Matumizi mazuri ya saa 24 za leo yatafanya upige hatua kadhaa mbele kuelekea mafanikio yako unayoyataka, kesho utaanzia pale ulipoishia leo kama leo utaitumia vizuri. Kesho itakulazimu upige hatua ya kwanza katika kukipata unachokitaka kama leo hauta leo itapita bila kufanya jambo la maana.

Rafiki mpendwa wangu, muda haumsubiri yoyote, unasonga mbele, hausimami kwa ajili ya yoyote wala chachote, haumjui yoyote, haumpendelei yeyote. Inuka, tupa shuka, zinduka…..fanya ukikumbuka uko nyuma ya muda hivyo inakupasa kukimbizana nao. Ni wakati wako sasa. Wakati wa ndoto zako. WAKATI NI SASA. MUDA WA KUFANYA CHOCHOTE UNACHOFIKIRIA NI HUU.

CHEMCHEMI3 BLOG@DARASA LA MAISHA#HOSPITALI YA MAISHA

 

Post a Comment

 
Top